TANGAZA NASI

Breaking

Ijumaa, 18 Desemba 2015

KHADIJA OMARY KOPA AMKANA HASSAN ALLY U-DIRECTOR WA BENDI NDANI YA OGOPA KOPA CLASSIC.

NA KAIS MUSSA KAIS.


                  Malkia wa mipasho nchini tanzania khadija omary kopa ambae ni mkurugenzi wa ogopa kopa classic bendi amemkana young hassan ally kuwa si director wa bendi kwa sababu director jukumu lake ni kujua maendeleo ya bendi, kama kuna nyimbo mpya ama kuna mazoezi ya umuhimu lakini si kwa hassan ally.
MALKIA WA MIPASHO NCHINI-KHADIJA OMARY KOPA.

       

            Aliyasema hayo wakati akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hizi katika tamasha la mitikisiko ya pwani ambalo lilifanyika wiki iliyopita katika ukumbi wa dar live mbagala jijini dar, bendi yangu haina director katika uongozi wa wasanii, hassan ally hajui mazoezi yanaendaje, hajui kuna nyimbo mpya, hajui kama kuna msanii mpya, haudhulii mazoezi sasa huyo utamuita ni director alihoji? sina director katika bendi yangu nasisitiza tena naomba nieleweke!.


YOUNG HASSAN ALLY.

           Mwandishi wa habari hizi alimtafuta hassan ally ndani ya ukumbi huo na kufanya mahojiano nae, kwa upande wake yeye alisema kuwa hakuwahi kutumiwa sms au kupigiwa simu kuambiwa issue ya mazoezi zaidi kuna siku aliandikiwa sms kuambiwa kwamba mtangazaji wa times fm dida anakuja mazoezini kwahiyo anatakiwa awepo, mimi nashukuru kama mama amesema hanitambui mimi kama director wa ogopa kopa, bendi ni yake na sisi ni wafanyakazi wake tu haina shida lakini anapaswa kutambua umuhimu wangu kwake!.Nasikia wimbo nilioutunga mimi "ushoga ndui" ambao uliimbwa na aziza kimiss na aziza bonge unafutwa na kuimbwa upya na zena mohamedy na mwamvita shaibu lakini...kwanini sishirikishwi? au kwavile mimi sio director?. haina shida mimi nipo ndani ya ogopa kopa na khadija kopa ataendelea kuwa mama yangu tu alimaliza kwa kusema.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni