Mpiga solo mashuhuri nchini tanzania katika tasnia ya muziki wa taarab jumanne ulaya "J4" amesimamishwa kazi kwa kipindi kisichojulikana baada ya kutofautiana na viongozi wake wa kolombwe modern taarab.
Uchunguzi uliofanywa na dawati la habari la mtandao huu ulibaini taarifa hizi baada ya kufanya upekupeku wake kutoka katika vyanzo vyetu vya habari ambavyo tunaweza kusema kuwa vimetapakaa katika bendi zote za taarab nchini tanzania. Taarifa zinasema kuwa jumanne ulaya amekuwa akilalamika kwanini awekwe katika kolombwe namba mbili na sio namba moja kutokana na hadhi yake aliyonayo katika muziki huu wa taarab nchini, alisikika akilalamika kuwa hii ni dharau kujumuishwa na hawa wasanii wachanga ambao sio hadhi yangu kabisa ni bora hata hii bendi ife tu!.
JUMANNE ULAYA AKIWAJIBIKA STEJINI. |
Kwahiyo jumapili ya wiki iliyopita wakati wanatoka katika show, kolombwe zote mbili zilikutana na ndipo mkurugenzi mkuu Babu chollo akatumia busara kwa kuwaambia wasanii wa kolombwe modern taarab namba mbili ambayo yupo jumanne ulaya kuwa kuanzia leo naivunja na wasanii wote mkatafute kazi sehemu ingine, lakini lengo lilikuwa ni kumuondoa J4 kibusara ili wasanii wenzake wasione kuwa kadharauliwa.
Jumanne ulaya alipofika nyumbani kwake na kutafakali kwa kina kauli ya mkurugenzi Babu chollo aliamua kumtumia sms mkurugenzi huyo ambayo ilikuwa ikisomeka kama ifuatavyo nanukuu:-
"Mtu wangu maamuzi yako yapo sahihi, tupo pamoja ila kukaa isiwe kigezo bendi zote za taarab nilishawahi kufanya hivyo, melody, jahazi na zingine zingine nyingi kwenye taarab. isitoshe hata mziki ulikuwa unapigwa unakatisha tamaa na nilikuwa hapa kwa kukuheshimu tu nna njaa nna dhiki sana sio kwa bendi na mziki huo maadamu tupo hai tutaonana ila imenifurahisha sana ili niondokane na kujichoresha na miziki ya akina yahaya".
BABU CHOLLO-MKURUGENZI WA KOLOMBWE MODERN TAARAB. |
Alipotafutwa jumanne ulaya ili ajibu haya aliyoyasema mkurugenzi babu chollo, yeye alianza kwa kusema kuwa hakuwa ameajiliwa pale kolombwe sasa wanawezaje kunisimamisha au kunifukuza bendi? alihoji, ile ni bendi ya ndondo tu ambayo msanii yeyote anaweza kwenda kupiga. unajua ndugu mwandishi nikwambie jambo moja bendi ile haina nidhamu kabisa, wasanii wake wanagombana steji kila wakati, walevi wana uwezo mdogo sana kulinganisha na mimi...siwezi kuendelea kujidhalilisha kwa kupiga katika bendi kama ile. kuna huyu jamaa anaitwa yunus sijui ndio nani...mimi simtambui anasema kuwa amenisimamisha bendi, yeye ni nani katika bendi? alihoji maana simtambui. waache waendelee ila mimi nakataa hawajanifukuza wala kunisimamisha kwani sina mkataba nao kabisa mimi alimalizia.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni