NA KAIS MUSSA KAIS.
Mtangazaji wa ras fm redio ya dodoma mwajuma isumail au kama wengi wanavyopenda kumuita kichuna toka mkoani morogoro leo kwa kujiamini kabisa amefunguka na kuweka wazi mahusiano yake ya kimapenzi na mtoto wa malkia wa taarab nchini khadija omary kopa aitwae "black kopa" na kusema anampenda sana!.
BLACK KOPA AKIWA NA MWAJUMA ISMAIL AMBAE NI MPENZI WAKE KWA SASA. |
Akizungumza na mtandao huu baada ya kuulizwa swali na mwandishi wa habari hizi kuwa kuna tetesi zimezagaa kwa wadau na mashabiki wa taarab nchini kuwa yeye anatoka kimapenzi na black kopa je ni kweli taarifa hizi?, mwajuma alianza kwa kucheka na kuitikia kwamba ni kweli taarifa hizo, akiendelea kulithibitisha hilo alisema, mapenzi yangu na black kopa sio kificho tena kwani mpaka familia yake black kopa wananijua na dada zake huwa wananiita wifi yao!, mama khadija omary kopa pia ananitambua kwahiyo sioni sababu ya kuficha mahusiano yetu, nampenda sana black kopa na sina mwanaume mwingine zaidi yake.
KIUKWELI WAMEPENDEZA SANA!. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni