TANGAZA NASI

Breaking

Jumanne, 10 Mei 2016

HASHIM SAID "MZEE WA MAJANGA" KIKAANGONI MBELE YA WATANGAZAJI JUMATATU IJAYO.

NA KAIS MUSSA KAIS.


HASHIM SAID "MZEE WA MAJANGA" AKIPOZI KWA PICHA.

          Group la watangazaji wa muziki wa taarab kupitia redio na televisheni jumatatu ya wiki ijayo watapata nafasi ya kufanya mahojiano na Hashim said au ukipenda muite 'mzee wa majanga' katika kile kipengele kinacho endelea kujizolea umaarufu cha "kikaangoni wiki hii".


        Hashim said ambae wiki iliyopita alitangaza rasmi kuipa kisogo bendi ya wakaliwao modern taradance atawekwa mtu kati na watangazaji zaidi ya tisini kwa maswali, watangazaji hawa wanatoka mikoa tofauti ya tanzania nikimaanisha unguja, pemba na mikoa ya tanzania bara, pia kuna watangazaji tokea nchini kenya ambao nao hupatikana humo. anachotakiwa kufanya hashim said ni kujibu maswali yote toka kwa watangazaji hao na muda ukifika wa yeye kuondolewa katika group hilo basi admin hufanya hivyo na kuwaacha watangazaji wakiendelea kupiga stori zao kama kawaida.


          Kubwa wapenzi wa blog hii ya ubuyu wa taarab kuweni tayari kusoma kile ambacho hashim said atakuwa ameulizwa na kuweza kujibu, hii ndio blog bora ya taarab kwa sasa hapa nchini tuendelee kuwa pamoja kwa maoni na ushauri wasomaji wangu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni