TANGAZA NASI

Breaking

Jumatano, 8 Novemba 2017

AMINA MNYALU:- KAMWE SIWEZI KURUDI MAJAZ MODERN TAARAB...HATA BURE!!.

Na pambe za taarab.

Muimbaji chipukizi anaefanya vizuri kwa sasa ndani ya bendi ya Tmk modern taarab Amina rashid a.k.a. Amina mnyalu ametoa la rohoni kwa kusema kuwa kamwe hayupo tayari kufanya kazi tena ndani ya bendi yake ya zamani ya majaz modern taarab.

Akizungumza na wadau ktk group la whatsap liitwalo pambe za taarab kwenye kipengele kiitwacho sindano za motto ambacho huwa kinakuwa hewani kila siku za jumatatu Amina aliongea hayo baada ya kuulizwa swali kuwa wakati majaz wapo safarini mpanda ilitokea sintofahamu akapigwa makofi na mkurugenzi wake je ni kweli?, ndipo Amina akaeleza  habari hizo ni kweli na kisa cha mimi kupigwa ni stori ndefu sana lakini sitoweza kuizungumzia, ila kwa tukio lile nimeapa kwamba kamwe haitotokea mimi kurudi tena kufanya kazi ktk bendi ile hata kama bendi za kwenda ziwe zimekwisha basi nibora nifanye biashara zangu tu.

Mwandishi wa habari hizi alijaribu kumtafuta mkurugenzi wa majaz ktk simu yake lakini hakupatikana hewani tutajitahidi kumtafuta ili tuweze kuwaletea nae anasemaje juu ya haya aliyoyazungumza Amina mnyalu yana ukweli kwa kiasi gani...tuendelee kuwa pamoja wasomaji wetu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni