TANGAZA NASI

Breaking

Jumanne, 20 Februari 2018

HASSAN VOCHA:- ABDALLAH FERESH NI ZAIDI YA MZAZI KWANGU!.

HASSAN VOCHA.
Na pambe za taarab.


Wakati said fellah ananitoa mkubwa na wanawe na kunipeleka pale G5 modern taarab kwake Hamisi slim sikutegeme kama siku moja nitakuja kukutana na Alhaji Feresh mtu muhimu kwangu ambae kwa kiasi kikubwa ni mzazi kwangu kwa maana amekuwa akinifanyia mengi sana ya kimaendeleo kama mwanawe.


Safari ya kimuziki ina mabonde na milima inatakiwa uwe mvumivu na busara ili uweze kufanikiwa, nilipofika pale G5 sikuwa mzoefu sana na muziki huu wa taarab isipokuwa kwakuwa nilikuwa muimbaji mzuri wa bongo fleva sikupata shida kuzoea mazingira haya. Kuna siku moja wakati nipo pale mazoezini G5 alikuja Adam mlamali huyu ni nguli wa muziki wa taarab ambae aliwahi kutamba na bendi za zanzibar stars na east african melody kipindi hicho, aliponiona nikiimba alivutiwa nami akaniomba ikiwezekana nijiunge dar modern mimi na msanii mwenzangu Hasna, nasi kwakuwa tulikuwa tuna nia ya kujifunza zaidi tulikubali nikiwa na mwenzangu Hasna.


Huo ndio ukawa mwanzo wa mimi kukutana na mkurugenzi wangu Alhaji Abdallah Feresh, tokea nimeanza kumfahamu nimekuwa ni mtu mwenye furaha kila siku kwani Feresh kwangu amekuwa ni kama mzazi haswa ukizingatia nimeondokewa na wazazi wangu hivyo amekuwa akinifariji sana na kunichukulia kama mtoto wake wa kunizaa! naweza kusema kuwa sijutii kumfahamu, amekuwa ni msaada mkubwa kwangu kuanzia kwenye sanaa mpaka katika maisha!, napenda nimpongeze Bosi wangu kwa kunijali na kutujali wasanii wote wa dar modern.


Mimi kwa upande wangu sifikilii kuhama dar es salaam modern taarab kwani hapa nakuwa kama nipo nyumbani, sina shida kabisa naishi kwa amani kabisa, kwa sasa muda na wakati wowote dar modern tutatoa nyimbo zetu mpya nami kuna kitu kipya kabisa nitakuja nacho hivyo wapenzi na wadau wangu wajiandae kwani mara zote huwa sibahatishi alimalizia kwa kusema Hassan vocha!.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni