TANGAZA NASI

Breaking

Ijumaa, 16 Februari 2018

PILI AOGWA KUHOJIWA NDANI YA GROUP LA PAMBE ZA TAARAB JUMAMOSI HII.

Na pambe za taarab.


Mdau mkongwe aliewahi kutamba sana katika tasnia ya watuma salamu ndani ya redio mbalimbali na pia ametajwa katika nyimbo kadhaa za taarab nchini Pili aogwa au ukipenda muite mrembo wa kigamboni jumamosi ya wiki hii anatarajiwa kuhojiwa ndani ya group la pambe za taarab "wadau" kuanzia saa moja kamili usiku mpaka mbili kamili.


Segment ya kijamvi cha motto ndipo ambapo atahojiwa mdau huyo mpole na asie na makuu, akizungumza na admin Shija muwakilishi wa ma-admin tokea mkoani dodoma Pili aogwa alisema kwanza amefurahi kupata nafasi hiyo adhimu na muhimu kwake ili kuwajulisha wadau wachanga nini maana halisi ya udau, na ni kwa vipi alifanikiwa kufahamika mpaka kupata heshima mbalimbali tokea kwa watangazaji wa taarab na wasanii mbalimbali hapa nchini.


Mtandao huu wa pambe za taarab una vyanzo vyake vya habari mbalimbali likiwemo hili group la wadau wa muziki wa taarab, group la watangazaji wa taarab nchini, magroup mbalimbali ya facebook kama kashda na raha za pwani, ubuyu wa taarab. Pages Pambe za taarab na nyinginezo.


PILI AOGWA AKIWA KATIKA BIASHARA ZAKE.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni