TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 25 Februari 2018

KIVURANDE JUNIOR "LIVE" NDANI YA SINDANO ZA MOTTO PAMBE ZA TAARAB WHATSAP GROUP JUMATATU.

Na pambe za taarab.


Ile segment pendwa inayowahusu wasanii wa taarab, kibao kata, segere, mduara, Baikoko na singeli iitwayo "sindano za motto" wiki hii Kivurande junior mfalme wa kibao kata ndio anawekwa kikaangoni na wanachama na wadau wa group hilo bora kabisa kwa sasa hapa nchini tanzania.


Akizungumza na mtandao huu admin msaidizi wa group hilo Aunty shija mwenye makazi yake dodoma nchini tanzania alisema kuwa Kivurande alipendekezwa na wanachama wa group hilo kuwa yeye ndio ahojiwe kwani wana maswali mengi sana dhidi yake ukizingatia kuwa yeye ndio mfalme wa kibao kata kwa sasa hapa nchini.
Nae Kivurande junior kwa upande wake alisema kuwa anawashukuru sana viongozi na wanachama wa group hilo la whatsap kwa kumpendekeza yeye kuhojiwa ndani ya group hilo, nimekuwa nikiiwania sana nafasi hii kwa muda mrefu sasa na nashukuru nimeipata kikubwa nawaahidi nitashirikiana nao vizuri kwa kujibu maswali yote na kamwe sitowaangusha alisema Kivurande junior.


Sindano za motto ni segment inayowahusu wasanii na kila siku ya jumatatu kuanzia saa moja kamili usiku ndio rasmi huanza hewani rasmi.


KIVURANDE JUNIOR AKIWA KATIKA POZI.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni