TANGAZA NASI

Breaking

Jumanne, 17 Machi 2020

BONGO STAR'S MODERN TAARAB KUISIMAMISHA DAR LIVE KTK UZINDUZI WA ALBAM YAO MPYA!


Na Kais Mussa Kais.


        Bendi yako ya Bongo stars modern taarab yenye maskani yake mbagala jijini dar ipo mbioni kuzindua albam yake mpya inayokwenda kwa jina la bahari ya huba siku ya ijumaa tarehe 20/3/2020 katika ukumbi wa dar live mbagala.

      Akizungumza na mtandao huu mkurugenzi mtendaji wa bendi hiyo Senior Bachelor alisema katika uzinduzi huo wameialika bendi ya mashauzi classic inayoongozwa na Isha mashauzi, seven survivor mnanda chini yake Baba Aminata, Segu segumbo mtaalam wa miondoko ya singeli, matarumbeta na burudani nyingi sana ambazo zitakufanya uendelee kuburudika kwa kila radha ya burudani.

Aliongeza kwa kusisitiza wadau na wapenzi wa taarab dar na vitongoji vyake kujitokeza kwa wingi kwani kiingilio cha show hiyo ni cha kawaida sana shilingi 5000/= kwa mtu mmoja, show itaanza saa mbili usiku hadi majogoo. show itaongozwa na Mc Dokta kumbuka, Mc Jojoo na Maite Hassan mtangazaji wa kipindi cha taarab city redio fm ya dar es salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni