TANGAZA NASI

Breaking

Jumatano, 18 Machi 2020

Corona yaahirisha safari ya Mzee Yusuph kurudi mjini.

Na kais Mussa kais.



         Hatimae ile hashtag ya narudi mjini aliyokuwa akiitumia mzee yusuph imesitishwa rasmi jana baada ya serikali ya jamhuri ya muungano kuzuia shughuli zote zenye mikusanyiko kwa mwezi mzima kuepuka maambukizi ya gonjwa la corona ambalo ni tishio kwa sasa ulimwenguni.

            Mzee yusuph alitumia mitandao yake ya kijamii kuwahabarisha wadau wake kwamba kutokana na maagizo ya serikali kusitisha shughuli zote za mikusanyiko mbalimbali kwa siku 30 ili kuepusha maambukizi ya gonjwa hili baya nchini, nae amesitisha kwa muda ujio wake mjini mpaka hapo baadae.

      Lakini aliendelea kusema kuwa atawekeza nguvu zaidi studio kurekodi nyimbo zake kwahiyo yeyote ambae atakuwa tayari kudhamini gharama za kurekodi basi awasiliane nae milango ipo wazi kabisa, huyo ndio mzee yusuph ambae watu walikuwa wakisubiri kwa hamu ujio wake mjini kila mmoja akisema lake juu ya ujio wake mpya.

Wakati huo huo serikali ya Jamhuri ya muungano wa tanzania kupitia kwa waziri mkuu amepiga marufuku matasha yote ya muziki nchini kwa muda wa siku 30 mpaka hapo litakapotoka tangazo lingine.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni