TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 13 Machi 2016

LEYLA RASHIDI:- SINA MUDA WA KUPOTEZA KUTUMA WATU WATUKANE MITANDAONI.

NA KAIS MUSSA KAIS.

           Muimbaji wa jahazi modern taarab na mke wa mfalme mzee yusuph, bibie Leyla rashid leo katika kipindi cha taarab ndani ya redio one stereo amesema kuwa hana muda wa kupoteza kutuma watu watukane mitandaoni.

LEYLA RASHIDI AKIWA NA MUMEWE MZEE YUSUPH.

          Akizungumza kwa njia ya simu na mtangazaji Rehema nyamaka wa redio one stereo, leyla alisema kuwa amechoshwa na taarifa hizo na asingependa kuzizungumzia sana kwani zinamchefua kama kutukanwa ameshatukanwa ila yeye anamuachia mungu tu, haoni sababu ya kujibu chochote kile juu ya hilo, mtangazaji rehema nyamaka alimuuliza leyla kama ni kweli mfalme mzee yusuph aliwaita wote wawili yaani yeye leyla rashidi na wifi yake khadija yusuph ili kuwapatanisha, leyla alijibu kwa ufupi tu kuwa sipendi kuzungumzia.

        Mtandao huu unaipongeza familia hii kwa sasa kwani hali ni shwari na kila mtu anaendelea na hamsini zake, pongezi kubwa ziende kwa Big daddy mzee yusuph kwa kutumia busara kubwa katika kulimaliza hili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni