Bendi yako ya dar es salaam modern taarab yenye maskani yake magomeni mikumi jijini, kwa sasa imeliteka jiji kwa show yake bab-kubwa! walioipa jina na "usiku wa jamvi la jiji" ambayo huwa inafanyika katika ukumbi wao wa dar modern hall kila siku ya ijumaa.
Akizungumza na mtandao huu msanii tegemeo wa bendi hiyo Hassan vocha alisema kuwa show hii ni tofauti na show zingine zote ambazo bendi zingine wanafanya, kwanza ukianzia kwenye mandhari yenyewe ndani ni kusafi sana kunanukia manukato, full A/C, huwa kunatandikwa majamvi mapya kabisa, na hata viti vilivyo pambwa vyema pia huwa vinakuwepo, kwahiyo wale wanaopenda kukaa chini huwa wanakaa na wale ambao wanapenda kukaa katika viti pia wanakaa, kwa upande wa toilet ni kusafi kupita maelezo, kila mtu anapotoka chooni basi kuna mtu maalum ambae huwa anakwenda kusafisha na kumwagia manukato.
MASHABIKI WAKISEREBUKA KATIKA USIKU WA JAMVI LA JIJI IJUMAA ILIYOPITA. |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni