KAPTEN TEMBA MKURUGENZI WA FUNGAKAZI MODERN TAARAB. |
Akizungumza kwa njia ya simu temba alisema huyo senior bachelor anatafuta kiki kupitia jina langu ila namuonya kuwa mimi sio level yake atafute watoto wenzie ajibizane nao mimi sina muda mchafu, ila kwa kumuonyesha kuwa mimi naweza nimeamua kutumia verse zipatazo mbili tu! ili ahangaike nazo.
Mashairi ya wimbo huo ni haya hapa na yanakwenda kama ifuatavyo:-
Umekwisha huna swaga, bora ukauze kuni
Maisha yamekupiga, umehamia ukweni
Kupenda kwako kuiga, inakushinda sabuni
Pasport yangu kubwa ntafika hadi marekani, ya mombasa yamnekupa shida
Kuropoka hauchoki, dereva wa bodaboda
Sasa kauze samaki, wewe mpakaa poda na kuvaa vitaiti
Yangu yatakupa shida, nnayo ya uturuki
Kama mie changu ndoa, mama yako tumuite nani?
Hakuwahi kuolewa, na morogoro anaishi na bwana
Kazaa watoto saba, na wote wa zinaa
Kwenu adabu hamna, wala hamkulelewa
Shida kwenu ipo sana, mtoto wa miaka kumi anaishi na bwana.
VERSE 2:- Kama wako katulia, mbona hukuukuta usichana?
Wapo walokuanza, twawajua kwa mapana
Pia wanaendelea, kama habari hauna
Mimba uliyoilea, nenda kajiulize sana
Nna mengi ya kuongea, mda mchafu sina
Kama ndoa tulioana sisi, maneno ya nini?
Kuachana pia tumeachana sisi, inakuhusu nini?
Usiseme ya wenzako, ya juu uloyaona
Pia nasi tuna yako, ya marefu na mapana.
Habari ndio hiyo, kama ambavyo niliwaahidi kuwaletea part 2 ya hili timbwili na kweli leo nimetimiza, mimi na wewe hatujui kikubwa ambacho wana gombea kapten temba na senior bachelor, katika hali ya kawaida tu ni ngumu kuamini kwamba hawa upinzani wao upo katika muziki tu! kuna mambo makubwa sana yamefichika baina yao, sababu senior bachelor amemuoa dada wa kapten temba, sasa jiulize kama ni shemeji yake ni nini haswa wanachogombea wawili hawa?, vuta subira utayajua kupitia hapa mtandaoni, endelea kufuatilia kisa hiki.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni