TANGAZA NASI

Breaking

Jumapili, 30 Julai 2017

TETESI:- WAIMBAJI WATATU WA OGOPA KOPA WAHISIWA KUTIMKA.......

Na pambe za taarab.

Bendi ya ogopa kopa classic inayomilikwa na malkia wa mipasho nchini khadija omary kopa inasemekana imekimbiwa na waimbaji wake watatu mahiri nao ni Mwamvita shaibu na Zena mohamedy ambao wanaonekana zanzibar stars na Naima mohamedy ambae anaonekana katika jukwaa la   jahazi modern taarab.

Kachero wetu alifanya mahojiano na kiongozi mmoja wa jahazi modern taarab ambae hakupenda kuwekwa wazi jin lake kwa kisingizio yeye sio msemaji wa bendi, kiongozi huyo alisema kuwa Naima mohamedy kwa sasa ni muimbaji wetu na yupo katika ratiba za kupewa wimbo mpya ndani ya bendi hii.

Kwa upande wa Mwamvita shaibu na Zena mohamedy wenyewe wamekuwa wakifichaficha kwa kusema kwamba wamekuwa wakienda katika show za zanzibar stars kwakuwa bendi yao ya ogopa kopa haina show kwa sasa na ukizingatia wao ni wasanii waandamizi wa iliyokuwa zanzibar stars kipindi hicho hivyo hawaoni ubaya kushiriki maonyesho yao. Habari zaidi za kiuchunguzi zinasema wasanii hao wamechukizwa baada ya kutegemea siku ya sikukuu ya Idd bendi ingesafiri kwenda mombasa kenya lakini matokeo yake ikawa kinyume na wasanii hawakusafiri.

Juhudi za kumtafuta mkurugenzi wa bendi hii malkia khadija omary kopa ili azungumzie sintofahamu hii zinaendelea, kikubwa tunawaomba wasomaji wetu tuendelee kuwa pamoja kwani mama mukubwa tutamtafuta athibitishe hili kwa kina zaidi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni