TANGAZA NASI

Breaking

Ijumaa, 17 Novemba 2017

HAMISI MAJALIWA:- SINA MUDA WA KUJIBISHANA NA YEYOTE MITANDAONI.

Na pambe za taarab.

Mkurugenzi wa maja's modern taarab Hamisi majaliwa amezungumza na mtandao huu wa pambe za taarab na kusema kuwa hana muda mchafu wa kujibishana na yeyote katika mitandao, mimi naangalia bendi yangu wapi inaelekea nini nifanye ili niweze kuboresha maisha ya wasanii wangu.

Mkurugenzi huyo aliyasema hayo pale alipoulizwa swali kuwa anazungumziaje tuhuma alizoshutumiwa na aliekuwa msanii wake Amina mnyalu ambae kwa sasa yupo kwenye bendi ya Yah tmk modern taarab, mnyalu alisema aliwahi kupigwa sana na majaliwa wakati wanatoka safari na maja's modern taarab na sababu ilikuwa ni baada ya mgeni kisoda Kuchukuwa pesa za majaliwa lakini kwenye kusafiri akaingia mitini na mnyalu ndie ambae alikuwa mdhamini wa kisoda kwenye kupewa pesa hizo.

Majaliwa alianza kwa kusema, mimi sio mtu wa kujibishana ktk mitandao na hata kama huyo Amina anasema kuwa mimi niliwahi kumpiga nadhani mngeenda kuuliza polisi maana hiyo ni kesi, mimi sina la kusema sipo tayari kumpa mtu kiki, na anaposema kuwa hayupo tayari kurudi maja's kwani nani kasema anamtaka?, mimi katika bendi yangu wala simfikirii kabisaa! katika majina ya wasanii. Unajua kuna majina ya wasanii ambao naamini hawa walikuwa muhimu kwangu na kwa bendi yangu ya maja's modern taarab mfano Young hassan ally, kibibi yahya, khanifa maulid, Marehemu nyawana fundikila, Aisha vuvuzella, mrisho rajabu, mwajuma kidoti, salha abdallah na senior bachelor hawa ndio wasanii ambao walipitia maja's na wengine bado wapo mpaka sasa na walikuwa na wana umuhimu mpaka leo kwangu na kwa bendi yangu hii, lakini mtu kama huyo Amina mnyalu wala sina muda na yeye sababu najua uwezo wake mdogo sana kwenye kuimba alisema majaliwa.

Habari hii ni kama mrejesho wa ile habari ambayo tuliwahi kuiandika hapa juu ya Amina mnyalu kusema yeye hana muda wa kurudi tena maja's modern taarab hata aambiwe bure ni bora kama bendi zote zimekwisha atauza biashara zake ndogondogo tu na hii ni baada ya kupigwa na mkurugenzi wake huyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni