TANGAZA NASI

Breaking

Jumatano, 27 Desemba 2017

TETESI:- JEURI YA FEDHA, WASANII WAWILI NGULI WA YAH TMK KUTIMKIA JAHAZI MODERN TAARAB?.

Na pambe za taarab.

Waswahili wanasema siku zote mwenye kisu kikali ndie mla nyama, kuna habari za kunyapianyapia zimetufikia kwamba jahazi modern taarab baada ya kuundwa bodi ya wakurugenzi imepania kuchukuwa msanii yeyote wanaemtaka na jeuri hiyo wanayo maana zimetengwa pesa zaidi ya milioni 30 maalum kwa kuiboresha bendi hiyo.

Mnyetishaji wetu aliendelea kumwaga unyunyu kuwa pale yah tmk modern taarab kuna wasanii wawili maarufu ambao wapo katika mazungumzo ya mwisho mwisho na matajiri hao wa jahazi modern taarab ambao wameamua kuja kuleta mapinduzi ya kweli katika muziki huu wa taarab nchini Tanzania na mambo yakisha kamilika watu wataacha midomo wazi kwa kushikwa na butwaa!.

Hawa mabosi wa jahazi modern taarab kwa pesa ambayo wamepanga kuwapatia wasanii wale wa yah tmk taarab ni vigumu kwa mtu mwenye akili timamu kuikataa hususani kipindi hiki ambapo karibia bendi zote zimekuwa zikilia ukata wa fedha kuwaandama alisema ripota wetu huyo.

Mtandao huu unayo majina ya wasanii hao nguli lakini ni mapema sana kuyaanika ni Sawa sawa na kuharibu usajili wa Dornad ngoma kutoka yanga kwenda simba! jambo kubwa lililo mbele yetu ni kusubili ili tuone nguvu waliyonayo matajiri hao wa jahazi modern taarab je ni kweli au tisha toto tu?...hiyo ndio taarab ya kisasa msanii unanunuliwa kwa fedha nyingi kama mcheza mpira wa miguu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni