TANGAZA NASI

Breaking

Alhamisi, 28 Desemba 2017

TETESI:- PRINCE AMIGO KUJIUNGA RASMI NA YAH TMK MODERN TAARAB SIKU YA BIRTHDAY YA BENDI.

Na pambe za taarab.

Muimbaji machachali prince amigo unatarajia rasmi kujiunga na bendi ya yah tmk modern taarab katika sherehe za kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa bendi hiyo ambayo itafanyika hivi karibuni hapa hapa jijini dar es salaam.

Akizungumza na mtandao huu makini wa pambe za taarab meneja wa bendi ya yah tmk modern taarab Said kessy alisema kwamba tayari tumeshafanya mazungumzo ya awali na prince amigo na tulipofikia kunaleta matumaini naamini kwa uwezo wa mungu tutamalizana nae kila kitu alichokuwa akikihitaji kabla ya sherehe yetu ya kuadhimisha birthday ya bendi.

Mtandao huu ulinyanyua simu na kumpigia prince amigo na kumuulizia juu ya issue hii ambapo alisema ni kweli viongozi wa yah tmk modern taarab walinifuata na kuniomba nijiunge na bendi yao na kuna baadhi ya mambo niliwaambia wanikamilishie ila mpaka sasa bado hamna chochote vijana wanasema ni sound tu!, mimi nina matarajio yangu brother nahitaji kuwa na bendi yangu mwenyewe mungu akijaalia so! muziki ni kazi yangu nafikili mpaka mwakani nitakuwa na la kusema zaidi tuombe uzima alimaliza kusema prince amigo.

Mtandao huu unawaahidi wasomaji wetu kuwa tutakuwa katika sherehe za birthday ya bendi hiyo ili kuona je ni kweli prince amigo atatangazwa kujiunga na yah tmk modern taarab ama lah!.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni