TANGAZA NASI

Breaking

Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Makala ya wiki. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Makala ya wiki. Onyesha machapisho yote

Jumanne, 17 Machi 2020

06:18

BONGO STAR'S MODERN TAARAB KUISIMAMISHA DAR LIVE KTK UZINDUZI WA ALBAM YAO MPYA!


Na Kais Mussa Kais.


        Bendi yako ya Bongo stars modern taarab yenye maskani yake mbagala jijini dar ipo mbioni kuzindua albam yake mpya inayokwenda kwa jina la bahari ya huba siku ya ijumaa tarehe 20/3/2020 katika ukumbi wa dar live mbagala.

      Akizungumza na mtandao huu mkurugenzi mtendaji wa bendi hiyo Senior Bachelor alisema katika uzinduzi huo wameialika bendi ya mashauzi classic inayoongozwa na Isha mashauzi, seven survivor mnanda chini yake Baba Aminata, Segu segumbo mtaalam wa miondoko ya singeli, matarumbeta na burudani nyingi sana ambazo zitakufanya uendelee kuburudika kwa kila radha ya burudani.

Aliongeza kwa kusisitiza wadau na wapenzi wa taarab dar na vitongoji vyake kujitokeza kwa wingi kwani kiingilio cha show hiyo ni cha kawaida sana shilingi 5000/= kwa mtu mmoja, show itaanza saa mbili usiku hadi majogoo. show itaongozwa na Mc Dokta kumbuka, Mc Jojoo na Maite Hassan mtangazaji wa kipindi cha taarab city redio fm ya dar es salaam.

Ijumaa, 18 Mei 2018

04:38

KHADIJA MBEGU CHIPUKIZI ANAE TINGISHA KWA SASA, JE UNAJUA ALIANZIA WAPI?.

Na pambe za taarab.

    Muziki wa taarab unazidi kushika kasi kwa sasa hususani baada ya kuendelea kuzaliwa bendi kadhaa ambazo nimekuja kuzidisha ushindani ambao ulionekana kupotea kipindi cha kati nazo ni first class inayoongozwa na Prince amigo, five stone iliyo chini ya Juma mkima, halichachi classic ambayo inaongozwa na Amour magulu na nyingi nyinginezo.

Jina la khadija mbegu au ukipenda unaweza kumuita "khadija kais" ni ingizo jipya kabisa katika tasnia hii, msichana huyu mwembamba mrefu kiasi na asiye na majivuno naweza kusema ni miongoni mwa wale waliojaaliwa vipaji vya kuimba na mwenyezimungu na anajua kutumia kipaji chake haswa akiwa stejini, mtandao huu ulimtafuta ili kupata mawili matatu tokea kwake na kwa bahati tulimkuta nyumbani kwao kwa wazazi wake mbagala jijini dar es salaam maeneo ya "kwa dumbalume" na mahojiano yalikuwa yalikuwa kama ifuatavyo:-

Pambe za taarab:- Habari yako khadija, sisi ni wandishi tokea mtandao bora wa taarab nchini tanzania, tunapenda kujua historia yako kimuziki maana wasomaji wetu wamekuwa wakihitaji sana kujua ni wapi umetokea maana wanaona umeibuka tu na kuanza kufahamika, ni wapi ulipoanzia mpaka kufikia hapo?.

Khadija mbegu:- Kwanza nianze kwa kuwashukuru kwa kunitafuta mpaka mmeweza kufika huku kwetu mbali kiasi hiki, mungu awabariki sana, mimi kiukweli sina muda mrefu katika muziki huu wa taarab, nilikuwa naupenda muziki huu toka zamani lakini sikuwaza kuwa ipo siku nitakuwa muimbaji kama hivi, ilikuwa siku moja nimeenda kusuka huku huku kwetu mbagala nikakutana na Salha abdallah yule aliekuwa mke wa hammer Q, sasa kuna wimbo ulikuwa ukiimbwa ktk redio nami nikawa naufuatisha aliponisikia akasema wewe msichana mbona unajua kuimba sana!, kwani unaimbia bendi gani? nikamjibu mimi nipo tu nyumbani wala siimbi popote, ndipo akaniambia kesho twende mazoezini kwetu wakaliwao modern taradance kwa thabit abdul akusikilize unaonekana una kipaji sana basi nami nikamjibu sawa haina shida.

Pambe za taarab:- Ekhe vipi sasa ulifanikiwa kwenda huko wakaliwao au uliingia mitini kwa hofu? funguka mama!.

Khadija mbegu:- Mwenzangu we acha tu!, nilienda ndugu yangu nilipofika thabit abdul akanipigia vyombo kwa mara ya kwanza nikaimba wimbo uitwao "fungu la kukosa" wa bendi hiyo hiyo wakaliwao. Aliponisikia akasema uwezo wangu bado ila niwe naenda mazoezini kila siku nitakuwa vizuri maana kipaji ninacho. Basi nikawa naenda mazoezini na siku zingine naenda mpaka katika show zao! Ila kuna siku sitoisahau tulikuwa tunafanya show pale magomeni maeneo ya mwembechai karibu na shekhe Yahya hussein, thabit alisema kuanzia siku hiyo nisipandishwe stejini wala nisiruhusiwe kuimba sababu sijui. Basi nikarudi nyumbani nikawa siendi tena nafanya issue zangu zingine tu hapa home.

Pambe za taarab:- Sasa ilikuwaje tena mpaka ukaibuka na kuanza kuwa maarufu wakati uliamua kukaa nyumbani khadija?.

Khadija mbegu:- Nakumbuka siku moja nilikutana na kaka kais mussa kais akaniuliza unaimbia bendi gani kwa sasa? nikamjibu kuwa nipo tu nyumbani sina bendi, akachukuwa simu yake hapo hapo akampigia mkurugenzi wa jahazi kolombwe Chollo akamwambia huyu khadija ni ndugu yangu mpokee na umpe kazi, basi hapo ndio ukawa mwanzo wa safari yangu ya mafanikio kiuimbaji. Nilikaa jahazi kolombwe kama miezi nane tu! nikawa vizuri haswa ndipo kaka kais mussa kais tena kwa mara ingine akanipeleka jahazi modern taarab yenyewe sasa baada ya wasanii wengine kuhama na mzee yusuph kuacha bendi.

Pambe za taarab:- Wakati unaenda jahazi modern taarab uliwakuta wasanii gani wakongwe? na vipi hukuhofia kwakuwa umeingia ktk bendi kubwa kuliko uliyotoka?.

Khadija mbegu:- Pale niliwakuta fatma Kasim, mwasiti kitoronto, Mishi zele, zubeda mlamali, Mossi suleiman na wengineo nakumbuka chipukizi nilikuwa peke yangu tu, nilipewa jukumu la kuimba nyimbo zote za fatma mcharuko ambae alikuwa amehamia yah tmk modern taarab, kiukweli nilizitendea haki nyimbo zile maana nilikuwa nikiziimba kama yeye mwenyewe haswaa! jambo ambalo liliniongezea umaarufu zaidi na jina langu kukuwa zaidi na zaidi. Nilianza kutafutwa na wandishi kwa mahojiano na interview mbalimbali za redio nilifanya za nchini na nje ya nchi.

Pambe za taarab:- Sawa sawa!, hapa kati tumepenyezewa ubuyu kwamba umeondoka jahazi modern taarab na unaonekana gusagusa min bendi huku pia ukionekana mazoezini kwa bendi mpya ya amigo first class modern taarab hapa ikoje?.

Khadija mbegu:- Ahsante sana kwa swali zuri sana ambalo nami pia napenda wapenzi na wadau wangu wajue, mimi ni msanii na bado nipo ktk kujifunza kama ambavyo nilikutana na Sada nassor akanipa ushauri. Nyimbo za zamani kama zilizoimbwa na akina fatma issa, malika, bi rukia na wengineo zina njia haswa za uimbaji na muimbaji bora wa taarab ni lazima aweze kuimba nyimbo zile, nami nilikuwa sizijui nikapelekwa gusagusa min bendi na kaka kais mussa kais ili nijifunze zaidi na nashukuru kwa sasa naziimba vizuri sana mpaka nimeshaanza kuwa na wapenzi pale gusagusa!, sasa pale first class nilizungumza na mkurugenzi wangu Hassan farouk akaniruhusu wala haina shida maana first class wanaimba taarab ya kisasa na gusagusa tunaimba old is gold ni vitu viwili tofauti kabisa!. Unajua watu siku zote wanapenda kuona mtu unaharibikiwa nasikia tayari wameanza kupandanisha maneno kwa viongozi wangu bila kujua nini kinaendelea na watu hao nawajua kwa majina sema sina muda wa kuwajibu nawaacha waendelee kuporojoka!.

Huyo ndie khadija mbegu au ukipenda muite khadija kais chipukizi mwenye ndoto ya kufika mbali kimafanikio ndani ya muziki huu wa taarab nchini tanzania, mtandao wa pambe za taarab tunamtakia mafanikio katika safari yake hiyo ya muziki na tunampa ushauri anatakiwa awe mvumilivu kwani sehemu yoyote yenye mafanikio mitihani ni kitu cha lazima inampasa apambane na amuombe mungu zaidi.

Jumatatu, 12 Februari 2018

00:27

SAKATA LA KHADIJA KOPA NA KAPTEN TEMBA KAMA LITAENDELEA KUACHWA LITAFIKA PABAYA!.

Na pambe za taarab.





Mtafaruku unaoendelea baina ya malkia wa mipasho nchini tanzania bibie khadija omary kopa na mkurugenzi wa fungakazi modern taarab Kapten temba wa kudaiana pesa za malipo ya nyimbo ambazo kwa madai ya Kapten temba anasema alimtungia muimbaji huyo nguli kwa makubaliano ya kulipwa lakini mpaka sasa hajalipwa, kama utaachwa pasipo kuingiliwa na busara kutumika utafikia pabaya sana na kufanya mchezo hata damu inaweza kumwagika kwa wapenzi na mashabiki kupigana.


Kapteni temba ameandika katika ukurasa wake wa facebook unaojulikana kwa jina la "karya temba" akilalamika kudhurumiwa pesa zake na malkia huyo ambazo walipatana baada ya kumtungia mashairi ya nyimbo zipatazo nne ndani ya bendi yake ya ogopa kopa classic, lakini jambo ambalo sisi kama mtandao wa taarab nchini tumeona si busara ni kauli na maneno makali yasiyo na tafsida ambayo Kapten temba ameyatumia kwa mama huyu alie na mashabiki wengi tanzania na nje ya mipaka ya tanzania unapomuita mtu mzima kama khadija omary kopa kuwa ni mtu dhuruma ni kumshushia hadhi yake, malkia huyu ni "icon ya tanzania" vile vile ni icon ya muziki wetu huu wa taarab kumdhalilisha katika mitandao kwa umri wake tunaona si vyema hata kama ni kweli malkia anadaiwa basi zipo njia sahihi ambazo zingeweza kutumika kwenye kudai haki hii anayoizungumza Kapten temba.


Ukimsikiliza malkia wa mipasho nchini tanzania bibie khadija omary kopa katika clip zake alizotuma kwenye group la fans wake whatsap anakiri kudaiwa pesa na kapten temba kiasi cha shilingi laki tatu na tayari mwanzoni kabisa alimtumia shilingi elfu hamsini na akamuomba hizo zingine amvumilie kwanza sababu anashughuli ya harusi hapa kati lakini itakapokwisha basi atampatia pesa zake zilizobakia lakini temba hakuonekana kuridhika na majibu hayo ya malkia ndipo akaanza kwenda katika redio mbalimbali kuomba interview ili amchafue malkia huyo lakini alikuwa akikataliwa kufanya mahojiano, anaendelea kusema malkia huyo kuwa juzi tu hapa kuna pesa akawa amepata na nia ilikuwa ni kumlipa Kapten temba lakini ajabu mara anasikia amechafuliwa huko mtandaoni kwamba anadaiwa na Kapten temba na amepanga kumdhurumu!, sasa mimi nasema muacheni aendelee kuandika mimi simjibu na wala sitompa pesa yake iliyobakia kwanza mpaka amalize kunichafua ndipo nami nitampa pesa zake maana ameandika huko facebook kwamba huo ni Mwanzo tu habari kamili zitakuja alimaliza mama huyo asie na makuu.


Ukiingia katika account ya facebook ya Kapten temba na kusoma alichokiandika na ukapitia comment za mashabiki utaelewa ni kwanini nilisema damu zinaweza kumwagika, mashabiki wa khadija omary kopa wamechukizwa sana kwa kitendo alichofanya Kapten temba kumdhalilisha malkia huyo mitandaoni hivyo wametokwa povu la maana vijana wanasema, sasa hapa imehamia kwa wapenzi na imekuwa vita baina ya wanaompenda Kapten temba na wale wanaompenda khadija omary kopa je tunaupeleka wapi muziki wetu wa taarab?, suruhu ilishindikana mpaka tuletane mitandaoni?, hapa ndipo ninapokumbuka haki za msanii kama chama cha muziki wa taarab nchini kingekuwepo haya yote yangemalizwa na hakuna ambae angejua. Mtandao huu unapenda kuwaomba wadau wenye hekima zao kuingilia kati tatizo hili na kulipatia ufumbuzi ili maisha mengine yaendelee kwa pamoja tunasema tunalaaini vitendo kama hivi ndani ya muziki wetu wa taarab nchini.

Jumanne, 6 Februari 2018

01:05

THABIT ABDUL "MKOMBOZI" MUASISI WA TARADANCE ALIEWATOA WAIMBAJI WENGI!.

Na pambe za taarab.

Kipindi naanza kulisikia jina la Thabit Abdul mtoto wa ilala ilikuwa ni pale TOT bendi enzi hizo akiwa na akina marehemu Banza stone bila kumsahau Leylah Hatibu wakifanya vizuri katika wimbo wa mtaji wa masikini ni nguvu zake na nyingine nyingi.

Naamini safari ya muziki ya Thabit Abdul haikuanzia hapo isipokuwa alianza chini zaidi kama ilivyo taratibu za wasanii wengi mpaka wanafikia mafanikio. Ila kwa mimi wacha nianzie hapo TOT maana naweza kusema ndipo mafanikio yake yalipoanza kuonekana, Msanii huyu kwa sasa naweza kudiriki kumuita ndio "mfalme halisi wa miondoko ya taradance nchini" amepitia bendi kadhaa za taarab tukiondoa dance ambapo alipita twanga pepeta, extra bongo bila kuisahau TOT.

Wakati marehemu Mariam hamisi anatokea five stars modern taarab na kujiunga TOT taarab pale alikutana na Director Thabit Abdul na akamtengenezea wimbo uliomrudisha katika ramani ya muziki huu wa taarab wimbo uitwao "sidhuriki na lawama" katika huu wimbo thabit Abdul alipiga kinanda na kuweka njia za uimbaji yaani melodie, mariam akaanza kutajika tena midomoni mwa wapenda taarab maana huu wimbo ulifanya vizuri sana, baadae Mariam na thabit walipanga kuandaa album yao binafsi ndipo alipomtengenezea wimbo mwingine nje ya TOT taarab uitwao "mti wa ridhiki upo kwa mungu" ambao nao ulikuwa moto si mchezo mpaka umauti unamfika mariam bado walikuwa hawajaweza kuitoa album hiyo.

Tukija kwa marehemu nyawana isale fundikira, thabit Abdul ndio mtu wa kwanza kabisa kugundua kipaji chake wakati anatokea tabora kuingia dar na akamtengenezea wimbo wake wa kwanza ambao ulimtambulisha kwa mashabiki uitwao "nipo kamili nimejipanga" hapa thabit kila kitu alifanya yeye kuanzia mashairi, uimbaji, muziki mpaka kupiga vyombo hapo ndipo utajua kuwa thabit ni mtu wa aina gani!, baadae wakati nyawana yupo tanzania motto modern taarab thabit alipendekezwa na nyawana aende akamtengenezee wimbo, kipindi hicho thabit yupo bendi ya mashauzi classic na alienda na kumtengenezea nyawana wimbo uitwao "behind the scene" au nyuma ya pazia kama ambavyo wapenzi wanauita, wimbo huu ulifanya vizuri mno katika vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini. Lakini kabla nyawana hajafariki thabit abdul alimtengenezea wimbo mwingine nje ya bendi ya T motto uitwao "shetani kataja jina" wimbo ambao mpaka sasa bado ni kipenzi cha mashabiki wa taarab.

Thabit abdul amewasaidia wasanii wengi mno hiyo ni mifano michache sana, mtu kama Aisha Othman Vuvuzella, Aisha mtamu kabisa, Asya utamu, Isha mashauzi, malkia khadija omary kopa na wimbo wa Full stop bila kusahau Mjini chuo kikuu, Hamuyawezi kondo, Mwalimu nassor na wengineo wengi sana!. Falsafa yake ya kuifagilia sana taradance ndio inayomfanya kuonekana ni tofauti na wenzie ingawa wapo wanaompa challenge mtu kama Chidy boy wa yah tmk na Ally J wa jahazi modern taarab ni wapinzani wake wakubwa katika upigaji wa kinanda.

Huyo ndio Thabit abdul mkombozi mkurugenzi wa wakaliwao modern taradance baba wa watoto watatu wakike Hawa, Radhia na Hafsa thabit, mtandao huu kama kawaida yake unampongeza kwa kile anachokifanya kuwainua wasanii wachanga na kufanya waheshimike zaidi katika tasnia hii ya taarab nchini.

THABIT ABDUL "MKOMBOZI" MKURUGENZI WA WAKALIWAO MODERN TARADANCE.

Jumatatu, 5 Februari 2018

00:02

WADAU WA MUZIKI WA TAARAB NCHINI, MNAONA TUENDAPO NI SALAMA?.

Na pambe za taarab.

Wadau mara nyingi wamekuwa na thamani kubwa sana katika kuliendea jambo lolote lile ili kuhakikisha mafanikio yanapatikana kwa haraka na udhibiti  mkubwa.

Katika siku za karibuni muziki wa taarab umekuwa ukionekana kukosa ule msisimko wake uliozoeleka na kufanya baadhi ya redio kuondoa vipindi vyake hewani kwa kukosa wadhamini, kuna baadhi ya redio mfano kings fm ya njombe tanzania wameondoa kabisa kipindi cha taarab na redio zingine watangazaji ndio wamepewa majukumu ya kutafuta wadhamini ili kuweza kufanya vipindi wanavyoviendesha kuwa na uhai zaidi.

Ndipo nilipotazama na kuuliza hivi wadau wa muziki huu wanaona thamani ya tasnia yao inavyoporomoka kwa kasi ya ajabu? na nini wanapanga kuhakikisha muziki huu haupotei kabisa masikioni mwa wengi?, zamani nakumbuka wadau wa muziki wa dansi walikuwa na uwezo hata wakumsimamisha msanii ambae alikuwa anaonekana anakwenda kinyume na sheria za bendi yao! vile vile hata kama kuna msanii wanamtaka basi wadau wanaweza kuchangishana pesa na kumchukuwa msanii huyo na kumjumuisha ndani ya bendi yao...huo ni mfano tu!.

Nikirudi kwenu ndugu zangu mnafikili nini kifanyike ili muziki wetu wa taarab urudi ktk thamani yake kama zamani enzi za akina marehemu Amina chifupa?. Kwa sasa muziki wetu umekosa mvuto na kuna maneno yanazungumzwa kwamba baadhi ya viongozi wa muziki huu hawapendani kabisa!, nafikili baada ya kuendelea kukaa kimya ni vyema mkaitisha kikao cha wadau wote nchini ili kuzungumzia mustakabari au mwenendo wa muziki wetu ni wapi unapoelekea na nini tufanye ili kuunusuru usiporomoke shimoni kabisa.

Hapa tusiangalie mdau wa bendi gani ila sote ni wamoja tujumuike kwa pamoja ili tulijadili hili, kuwepo na semina elekezi pia kwa viongozi wa muziki huu ili kuwakumbusha kuwa upendo ni kitu bora na upendo unaleta maendeleo ya jambo lolote lile naamini tukifanya haya kwa kuanzia tunaweza angalau kupiga hatua kidogo. Mwisho kabisa tuamini kuwa sisi wadau ndio muhimili mkubwa wa kuifanya taarab iendelee kuwa juu zaidi na zaidi...mapambano bado yanaendelea!.

WAPENZI WA TAARAB WAKISEREBUKA.

Jumatatu, 23 Oktoba 2017

04:49

IPO HAJA BARAZA LA SANAA TANZANIA "BASATA" KUINGILIA KATI MCHAKATO WA KUANZISHA CHAMA CHA TAARAB NCHINI.

NA KAIS MUSSA KAIS.



      Wasomaji wangu wa blog bora kabisa ya taarab nchini tanzania ubuyu wa taarab nawakaribisha kwa moyo mkunjufu katika sagment hii ya makala ya wiki nami kais mussa kais kama ilivyo ada!.

     Lililo mezani leo hii ni kuhusu mchakato mzima wa kuanzisha chama cha muziki wa taarab nchini tanzania, ambalo naweza kusema kuwa wadau na viongozi wa bendi za taarab wameshindwa kabisa kuufufua umoja huu ambao hapo kabla uliasisiwa na wakongwe wetu akina mzee muchacho na wengineo, ni zaidi ya mara nne viongozi wa muziki huu wa taarab wameitana ili kuzungumza namna ya kuurejesha umoja huu lakini bila mafanikio.

     Viongozi wa muziki huu wa taarab nchini wamekuwa wabinafsi na hawajali maslahi ya wengine hususani wasanii wao, nawapongeza Amin salmin na Siza mazongela ambao walijitahidi sana kufuatilia usajili wa zamani waliosajili wazee wetu na kuweza kupatiwa mpaka katiba ambayo wazee wetu waliiwakilisha pale Basata "nakala ya katiba hiyo ninayo" ili waweze kutengua baadhi ya vifungu ambavyo vilikuwa vimepitwa na wakati na kuweka vya kisasa ili kuendana na wakati.

     Katika vikao vya kuijadili katiba hiyo ya zamani pale travetine magomeni viongozi wa bendi za taarab walipewa taarifa lakini hawakutokea kabisa, nakumbuka watu ambao tulikuwepo pale ni mimi mwenyewe, mkurugenzi wa kongamoyo taarab Iqubar, mkurugenzi wa T motto Amin salmin, mkurugenzi wa segere Siza mazongela pamoja na mdau mkubwa wa taarab nchini Emanuel kalugira, kwa mtazamo wa haraka haraka utagundua kulikuwa na mapungufu makubwa kwa baadhi ya bendi kukosekana katika kikao hicho pasipo sababu yoyote.

    Huu ni udhaifu na ubinafsi uliopo kwa baadhi ya viongozi wa taarab nchini, mnataka kusema kuwa hamjui umuhimu wa kuwa na chama katika muziki huu wa taarab ama lah?, chama cha muziki wa taarab ni muhimu sana katika kutetea haki zenu, mfano sasa hivi vituo vya redio vimepelekewa barua na serikali ili kuanzia tarehe moja mwezi wa nne waanze kuwalipa kila wanapocheza nyimbo zenu, lakini taarifa zilizoufikia mtandao huu ni kwamba kuna baadhi ya redio zinataka kugoma kucheza nyimbo za taarab sababu wanasema hawana pesa za kuwalipa!, naamini katika hili viongozi wa taarab ndipo utakapowaona unafiki na ubinafsi wao! wapo ambao watasema hawataki kulipwa pesa yoyote na nyimbo zichezwe tu! na wapo ambao watajaribu kugomea hili japo ni wachache, hapa ndipo unapokuja umuhimu wa chama cha taarab tanzania!.

    Chama kingekuwa hai utetezi ungepatikana na kila kitu kingekuwa sawa ila kwa vile viongozi wa taarab ni wabinafsi ndio maana sasa wanaburuzwa na wataendelea kuburuzwa sana huku haki zao zikipotea.

    Ushauri wa mtandao huu ni kwamba tunashauri na kuomba baraza la sanaa tanzania kuingilia kati na kusimamia kuanzishwa kwa chama hiki cha taarab tanzania, na hii ni kwa faida ya wasanii husika maana wao ndio wavuja jasho wanaostahiki faida za chama hicho, lakini kwa nguvu ya viongozi imeshindikana kabisa!, Basata tunaomba hili mlipe kipaumbele na mlifanye kwa haraka ili pia kunusuru haki za wasanii wa taarab nchini, kwa leo ni hayo tu tukutane tena wiki ijayo...Ahsanteni!.

Jumapili, 6 Agosti 2017

03:13

VIONGOZI WA JAHAZI MODERN TAARAB MSIPOKUWA MAKINI BENDI MTAIZAMISHA KWENYE TOPE!...

MAKALA MAALUM.
Na pambe za taarab.
Kuna ule msemo wa kiswahili usemao "ulie okota nae kuni ndio wakuota nae motto" hapa wahenga walikuwa na maana kubwa sana, ukiuchunguza kwa makini msemo huu utapata maana na utang'amua jambo la hekima sana!.
Katika siku za hivi karibuni kumezuka vikao vinavyofanyika kisirisiri ambavyo nia na madhumuni yake ni kufanya mageuzi katika uongozi wa jahazi ulio madarakani na kuurudisha ule uongozi wa zamani...hili sio baya kufanyika kama mkurugenzi mkuu anaona mwenendo wa viongozi wake wa chini haupo sawa! anaweza kuongeza nguvu ili kunusuru bendi kutetereka. Lakini huwezi kufanya vikao vya siri pasipo kuwa shirikisha wale uliowapa dhamana ya kuongoza, hapa utakuwa huwatendei haki na utakuwa umewadharau sana zaidi ya sana!, binadamu kukosea ni kawaida na kama unahisi hawapo sawa unaweza kuwaita na kufanya nao kikao cha kuwakumbusha ni nini wanatakiwa kufanya ili bendi ipate mafanikio.
Mtandao huu wa pambe za taarab upo katika kuuinua muziki huu kwahiyo linapokuja suala la kuudidimiza muziki huu kamwe hatuwezi kuufumbia macho ni lazima tuseme ingawa inaweza kuonekana baadhi ya viongozi watachukia kwa hiki kilichoandikwa lakini habari ndio hiyo. Kwa sasa ndani ya bendi ya jahazi modern taarab kumezuka sintofahamu kati ya mkurugenzi mkuu na viongozi wake wa chini, uchunguzi wa kina uliofanywa na mtandao huu na kujiridhisha unaonyesha mkurugenzi ameanza vikao na baadhi ya viongozi ambao walimsaliti na kumkimbia na kumuacha dhalili huku wakitoa kashfa kubwa kwamba jahazi limezama na hakuna wakuliinua tena, watu wamepata shida, wameishi maisha ya tabu kwa kujinyima ili jahazi lisimame na kweli mwenyezimungu kajaalia jahazi kwa sasa limesimama na wanafanya show mara nne kwa wiki, leo hii mkurugenzi anataka kuwaondoa wale aliopata nao shida na kuwarudisha wale wasaliti...hii haiko sawa!, ndio pale niliposema "ulie okota nae kuni, ndio wakuota nae motto".
Mkurugenzi kabla haujaanza kufanya chochote katika hayo uliyoyadhamilia napenda nikueleze yafuatayo, kwanza viongozi ambao umeplan kuwaondoa nafsi zao zimekunja kifupi hawajaridhika na unachotaka kufanya, pili kumbuka nguvu zao walizopoteza katika kupigania bendi isimame, wametoa nguvu zao, wametoa muda wao, wametoa pesa zao na vitu vingine si uungwana kuwaengua kwa dharau kiasi hicho!, hao unaowakumbatia sasa kumbuka ndio waliokukimbia na kukupa maneno mengi ya dharau na kashfa...leo hii umesahau?, Jahazi mpaka hapo ilipofikia sio kwa uwezo wako binafsi, mawazo yenu kwa pamoja katika vikao vyenu vya uongozi ndio vimeifikisha hapo jahazi mpaka hao wengine wanatamani kurudi...hebu kaa na ufikilie mara mbili upo sahihi kwa unachotaka kufanya au?...Geuka nyuma na kumbuka ulipotoka na unapoelekea naamini utagundua tatizo...Alamsiki!.